c Kum 7:23-24; 31:3; Yos 3:11; Kut 15:7; 19:18; 23:31; Ebr 12:29; Mik 2:13; Ufu 19:11-15; Isa 30:27; 33:14; Nah 1:5, 6; 2The 1:8; Kut 23:31
d Kum 8:17; 18:9-14; 2Fal 16:3; 17:8; 21:2; Ezr 9:11; Kut 23:24; Law 18:21-24, 30; Eze 36:32; Rum 11:6; 1Kor 4:4; Mwa 15:16
Deuteronomy 9:1-6
Si Kwa Sababu Ya Haki Ya Waisraeli
(Kutoka 32:1-35)
1 aSikiliza, ee Israeli. Sasa mnakaribia kuvuka Yordani mwingie na kuwafukuza mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi pamoja na miji mikubwa yenye kuta zilizofika juu angani. 2 bWatu ni wenye nguvu na warefu, ni wana wa Waanaki! Mnafahamu habari zao na mmesikia inavyosemekana: “Ni nani awezaye kusimama dhidi ya Waanaki?” 3 cKuweni na hakika leo kwamba Bwana Mwenyezi Mungu wenu ndiye atakayetangulia kuvuka mbele yenu kama moto uteketezao. Atawaangamiza; atawatiisha mbele yenu. Nanyi mtawafukuza na kuwaangamiza mara moja, kama Bwana alivyowaahidi. 4 dBaada ya Bwana Mwenyezi Mungu wenu kuwafukuza mbele yenu, msiseme mioyoni mwenu, “Bwana ametuleta hapa kuimiliki nchi hii kwa sababu ya haki yetu.” La, ni kwa sababu ya uovu wa mataifa haya ndiyo Bwana anawafukuza mbele yenu. 5 eSi kwa sababu ya haki yenu wala uadilifu wenu kwamba mtaimiliki nchi yao; lakini kwa sababu ya uovu wa mataifa haya, Bwana Mwenyezi Mungu wenu atawafukuza mbele yenu, ili kutimiza lile alilowaapia baba zenu Ibrahimu, Isaka na Yakobo. 6 fBasi mjue, si kwa sababu ya haki yenu Bwana Mwenyezi Mungu wenu anawapa nchi hii nzuri kuimiliki, kwa kuwa ninyi ni taifa lenye shingo ngumu.Ndama Ya Dhahabu
Copyright information for
SwhKC